DC MTATIRO AMALIZA MGOGORO WA ARDHI WA ZAIDI YA MIAKA18,NYUMBA YABOMOLEWA AMKABIDHI MMILIKI HALALI
Utekelezaji wa uamuzi huo umefanyika chini ya uangalizi wa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro, akishirikiana na askari pamoja na viongozi wa serikali za Mtaa waliokuwa wakihakikisha taratibu zote zinafuatwa.
Chanzo cha mgogoro huo kilianzia mwaka 2007 baada ya Boaz Mwaipopo kudai umiliki wa eneo hilo na kujenga nyumba, madai ambayo yalipingwa na familia ya Kulinga, wakieleza kuwa ardhi hiyo ni mali ya Dotto Pamela Zakaria Kulinga tangu mwaka 1992.
Akizungumza baada ya utekelezaji huo, Baraka Chande Kulinga amesema licha ya kuwa na nyaraka halali za umiliki, walilazimika kupitia mchakato mrefu wa kisheria ili kuthibitisha haki yao, akisisitiza umuhimu wa wananchi kuwa na uelewa wa sheria za ardhi.
Alibainisha kuwa mahakama ilitoa agizo Mei 16, 2025 likimtaka Mwaipopo kuondoka ndani ya siku 14, lakini alishindwa kutekeleza amri hiyo na kuendelea kuishi katika eneo hilo hadi ilipofikiwa hatua ya kuondolewa kwa nguvu kwa mujibu wa sheria.


0 Comments